Hansard Summary

The speaker emphasized the deep historical, cultural and ecological bonds between Kenya and Tanzania, arguing that cooperation is a natural and necessary outcome of shared heritage. He presented trade and investment data to illustrate growing economic interdependence and called for deeper collaboration, while sharply criticizing those who view the two countries as rivals. The Tanzanian Speaker expressed deep gratitude for the warm reception by Kenya, marking his first official visit and emphasizing the historic significance of the bilateral engagement. He highlighted the strong friendship, cultural ties, and collaborative discussions that fostered optimism for future cooperation, while noting that any minor differences are merely perspective‑based. The speech underscored a commitment to continued dialogue and joint initiatives between the two nations. The Speaker highlighted the importance of deepening Kenya‑Tanzania cooperation across trade, tourism, security and joint infrastructure, citing projects like the Lamu‑Mombasa to Tanga‑Bagamoyo road corridor. He stressed that collaborative efforts bring peace, economic growth and mutual benefits for both nations before adjourning the session.

Sentimental Analysis

Positive

THE PARLIAMENT OF KENYA

THE SENATE

THE HANSARD

PARLIAMENT OF KENYA

JOINT SITTING OF THE NATIONAL ASSEMBLY AND THE SENATE

Wednesday, 5th May, 2021

ARRIVAL OF HER EXCELLENCY THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

CONVOCATION MKUSANYIKO WA KIKAO MAALUM CHA BUNGE

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Your Excellency, hon.

(Applause)
(Applause)
(Applause)
(Applause)

ADDRESS BY VISITING DIGNITARY ADDRESS BY H. E. SAMIA SULUHU HASSAN, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Ninatambua kwamba huu sio utaratibu wa kawaida wa Kenya. Sio kila Rais anayefanya ziara rasmi hupewa heshima hii ya kuhutubia Bunge, tena Kikao cha Pamoja cha mabunge yenu mawili. Wenzetu mna Bunge lenye Chambers mbili, sisi wenzenu tuko na Bunge moja tu.

Kwangu, itakuwa ndio mara ya kwanza kuhutubia Chambers mbili za Bunge kwa pamoja. Sio jambo ndogo na ni heshima kubwa iliyoje. Mmenipa heshima kubwa sana. Nimefarijika kuwa nimepata nafasi hii mwanzoni mwa uongozi wangu. Niseme kuwa kumbukumbu hii haitafutika kwenye maisha yangu. Asanteni sana!

(Heko) Uamuzi wenu wa kunipa fursa hii ni kielelezo cha thamani na uzito ambao mnaupa uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi zetu mbili. Niwahakikishieni kuwa nasi tumeguzwa sana na heshima, upendo na ukarimu mkubwa ambao mmetuonyesha. Wema huacha deni na deni lake ni kulipwa kwa wema. Sisi Tanzania, tutalipa wema huu.

Waheshimiwa Maspika, Maseneta na Wabunge, sitatenda haki nisipomshukuru kipekee ndugu yangu, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta. Rais Kenyatta ni miongoni mwa viongozi wa mwanzo kabisa walionipigia simu kunifariji mara tu baada ya kusikia taarifa ya kifo cha aliyekuwa Rais wetu mpendwa, Hayati Mhe. (Dr.) Magufuli.

Kama haikutosha, hakusita kukatiza ratiba yake na kufika yeye binafsi kushiriki nasi katika msiba wa kitaifa kule Dodoma. Siku ile, alitufariji sana kwa maneno yake na salamu zake za buriani kutoka kwa wananchi wa Kenya. Hatutasahau pia kitendo chake cha kutukumbusha umuhimu wa kuheshimu dini na imani za wengine.

(Heko) Mhe. Uhuru Kenyatta alisitisha kuhutubia akiwa jukwaani, ili kupisha adhan iliyokuwa ikisomwa Msikitini imalizike na ndio akaendelea. Alituwachia gumzo na funzo kubwa sana kwetu. Alitumia jukwaa lile kunipongeza kwa kushika dhamana hii ya Urais ya Awamu ya Sita ya Tanzania. Aliahidi kunialika nchini Kenya mara baada ya kipindi cha maombolezo kumalizika.

Rais Kenyatta ni mtu wa kutimiza ahadi. Mara tu baada ya kumalizika kipindi cha maombolezo, alinitumia ujumbe maalum kuniona, ambao pia uliambatana na mwaliko wa kutembelea Kenya. Na mimi nimekuja Kenya kuitika wito wake.

Mimi na ujumbe wangu tumepata mapokezi mazuri sana toka tulipowasili Jijini Nairobi. Tumejisikia tuko nyumbani haswa. Tumepokewa kwa ukarimu mkubwa na hio ndio hulka, desturi na asili ya watu wa Kenya.

Nimebaini kuwa sehemu kubwa ya ujumbe nilioambatana nao, wanajua vichochoro vya Jiji la Nairobi. Wanajua nyama choma inapatikana wapi. Lakini kutokana na Korona, hawakuweza kujibamba. Nina wasiwasi nisije nikawabakisha nyuma.

(Kicheko)

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Tunawashukuru kwa yote; mapokezi na ukarimu mkubwa.

Jana nilifanya kikao na Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta na ujumbe wake wa viongozi wa Serikali. Tumekuwa na mazungumzo mazuri yenye kuamsha matumaini makubwa kwa mashirikiano kati ya nchi zetu mbili kwa siku zijazo mbele yetu.

Hapakuwa na ugumu wala ukakasi wowote katika kufikia mwafaka wa mambo tuliyokuwa tukijadiliana. Tumezungumza kwa kindugu sana. Kilichojitokeza wazi katika mazungumzo yale ni namna ambavyo nchi zetu mbili zinakubaliana katika mambo mengi kuliko yale machache sana tunayotofautiana.

Hata hayo machache tunayotofautiana, yenyewe hayakuwa na misingi imara ya tofauti ila ni mitazamo tu ya watu. Mitazamo nyingi ambayo inaleta ukakasi huchangiwa kutokana na kukatika kwa mawasiliano baina ya nchi zetu mbili. Sasa ili kuondoa mikakati hasi kati yetu, tumekubaliana kujenga na kuendeleza utamaduni wa kukutana mara kwa mara katika ngazi zetu mbali mbali. Ndugu na jirani wanaotembeleana hujenga ukaribu kuliko wale wasiotembeleana. Umbali hujenga mashaka na ukaribu huondosha mashaka hayo.

Waheshimiwa Maspika, Maseneta na Wabunge, kama nilivyosema, hii ni ziara yangu ya kwanza rasmi nchini Kenya tangu kushika wadhifa wa uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 19.03.2021.

Ipendeze kusema kuwa itaingia katika kumbukumbu za kihistoria kuwa Kenya ndio nchi ya kwanza kwa raisi wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya ziara rasmi. Nilikwenda Uganda kwa mathumuni maalumu ya kusaini mktaba.

(Heko) Haikuwa ziara rasmi. Ziara yangu rasmi ya kwanza nimeanza na Kenya. Kwa lugha nyingine, mguu wangu wa kwanza kutoka nje kwa ziara rasmi umeanza Kenya.

Jana nilikaribiswa Iftar na Mheshimiwa Rais na baadaye tukawa na chakula cha usiku. Dua nyingi zilisomwa na baada ya kumaliza kusoma dua, mvua ilinyesha. Ilikuwa baraka sana. Mungu ameweka baraka kwenya ziara yangu na yale yote ambayo tumezungumza. Kwa hivyo, tumshukuru Mungu.

Uamuzi wangu wa kuja Kenya, kuwa nchi ya kwanza, sio wa bahati mbaya wala ni wa makusudi. Busara inaelekeza kuwa ukiwa mpangaji mpya kwenye eneo, lazima ujitambulishe kwa majirani.

(Kicheko) Nami kwa sababu ni mpangaji mpya kwenye hizo nafasi, nimeonelea nije kwa majirani kujitambulisha na nimeanza na jirani wa Kenya ambaye ni jirani ndugu. Nilipata mialiko mingi lakini nilisema eti nianze na hapa. Sijaanza na Kenya kwa sababu ni karibu kijografia, bali ni kwa sababu ya umuhumi na nafasi ya Kenya kwa Tanzania.

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Uhusiano wa Tanzania na Kenya ni wa kipekee sana. Ni uhusiano uliofungwa katika mafundo matatu. Fundo la kwanza ni undugu wa damu kati ya wananchi wetu wa pande mbili ambao hauwezi kutenganishwa na mipaka ya kuchorwa kwenye ramani.

Makabila ya pande mbili za mpaka yanaingiliana na watu wake ni wale wale wamoja. Tanzania inapakana na nchi nane, lakini ni nchi ya Kenya pekee ndio ambayo tunajamii nyingi zilizopo katika pande mbili za nchi zetu.

Kwenye Ukumbi huu wa Bunge, nadhani ndani hapa kuna akina Otieno, Boke, Namelok kama ilivyo Tanzania. Lakini pia kuna akina Kilonzo na Kioko kama ilivyo Tanzania.

(Kicheko) Lakini zaidi, kuna Mohamed Faki Mwinyihaji ambaye ni Seneta wa Mombasa na jina lake ni jina safi la Kizanzibari. Kwa hivyo, hatuwezi kutengana. Hiyo ni mifano chache tu.

Fundo la pili ni historia. Kabla ya kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, 1967, nchi zetu mbili hizi tayari zilisha kuwa chini ya East Africa Common Service Organization (EACSO) zikiwa chini ya utawala wa Kikoloni wa waingereza. Huduma zetu muhimu, miundo mbinu yetu na uchumi zetu, zilifuma pamoja kabla hata nchi zetu hazijapata uhuru.

Fundo la tatu ni jiogrofia. Mwenyezi Mungu amejalia nchi zetu mbili hizi kuwa majirani. Tuna mipaka ya baharini na mipaka ya ardhini. Na hata ekolojia yetu ni moja. Ndio kusema kuwa hata wanyama pori wetu ni ndugu na ni majirani. Kuna wale wanyama pori ambao huja kupata mimba Kenya na wanarudi kuzaa Tanzania.

(Kicheko) Ingekuwa wanyama wana uraia, wangekuwa raia wa wapi? Wakitoka Serengeti, hao huingia Maasai Mara. Hata tausi wetu walioko Ikulu Tanzania, wana ndugu zao Ikulu ya Nairobi. Kwa hivyo, kama tausi na wanyama wana undugu, sisi wanadamu tunatengana wapi? Hatuna pa kutengana.

Kutokana na ukweli huo, ushirikiano wetu sio wa hiari bali ni wa lazima kutokana na kanuni ya uasili wa undugu ambao Mwenyezi Mungu ameumba. Ushirika na ujirani yote yanatufanya tuwe pamoja. Hali ya maumbile, hatuna uwezo wa kubadilisha. Iliyobaki ni tupendane au tuchukiane, tuzungumze au tununiane, hatuwezi kukwepa kutokana na mafundo hayo matatu tuliyowekwa nayo pamoja.

Tunategemeana kwa kila hali. Iwe heri au iwe shari. Iwe neema au dhiki, tunategemeana. Panapotokea ukame Tanzania, njaa inabisha hodi Kenya. Uzalishaji wa viwanda ukisimama Kenya, bidhaa zinakosekana Tanzania. Kwa hivyo, tunategemeana. Hivyo, hapana budi ila tupatane na tuelewane ili tuishi kwa pamoja kwa neema na furaha.

Waheshimiwa Maspika, Maseneta na Wabunge, binafsi huwa nashangazwa sana na wale ambao wanadhani eti Kenya na Tanzania ni washindani, kwa hivyo, uhusiano wetu unapaswa kuwa wakuhasimiana na kukamiana.

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Nawashangaa wanaodhani kuwa Kenya pekee yake ama Tanzania pekee yake inaweza endelea bila mwenzake. Mbaya zaidi ni kule kuamini kwao ya kwamba hiyo inawezekana tu mmoja wetu kumuangusha mwenzake. Hawa ni watu wenye mioyo ya choyo, maono mafupi na akili mbovu.

Ni bahati mbaya kuwa watu hawa wapo katika pande zote mbili; Kenya na Tanzania. Hutokea pia wachache wao sana wakawa ni watumishi wa Serikali zetu na hata wanasiasa wa pande mbili za nchi zetu.

Bahati kubwa ni kuwa, sio wengi na ndiyo maana uhusiano wa nchi zetu mbili unatimiza miaka 56 sasa. Ukiwacha ule uwasili, lakini ule wa kiserikali ni miaka 56 sasa.

Kwangu mimi na katika awamu yangu ya uwongozi, nitahakikisha kuwa Kenya inabaki kuwa ndugu, jirani, mshirika wa mkakati na mbia. Kenya ni nchi ya tano kwa nchi zinazoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania na ndiyo nchi ya kwanza ndani ya Afrika inayoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania.

Nyuma ya mataifa makubwa kama Uingereza, Marekani, China na India, inakuja Kenya. Ya kwanza kituo chetu cha uwekezaji zinaonyesha ya kuwa hadi kufikia Machi, 2021, kuna miradi mingi tu ya Kenya inayotekelezwa Tanzania kama Tshs500,013,000 kutoka Kenya ambayo inatekelezwa Tanzania na kutoa ajira kwa Watanzania Tshs51,187,000 na kuchangia mapato ya kiasi cha US$1.7 billion.

Sekta zinazoongoza kwa uwekezaji kutoka Kenya yaani uzalishaji viwandani, usafirishaji, kilimo, huduma, benki, ujenzi, rasilmali watu, madini, utalii na mali asili. Kutokana na uhusiano wetu mzuri, kampuni za Tanzania zimewekeza nchini Kenya lakini tumekuja kwa uchache sana. Tuko kama kampuni 25 mpaka 30 zilizosajiliwa na mamlaka ya uwekezaji ya Kenya.

Miradi hiyo ina dhamani ya Kshs19.33 billion na kutoa ajira kwa raia kama 2,642. Kwa hivyo, Tanzania tuna deni kubwa kuja Kenya lakini pamoja na mapungufu hayo tuliyo nayo, bado tunawaalika Wakenya wengi zaidi waje Tanzania kuwekeza.

(Heko) Tunawaalika kwa sababu Tanzania ina mambo mengi; ina rasilmali za kutosha, madini ya kutosha, ardhi kubwa na mambo mengi mengine,tunakosa mtaji. Kenya mna mtaji wa kutosha. Karibuni Tanzania.

Dhamira yangu ya kuja nchini Kenya ni kuzungumza na nyinyi na kuona namna gani Watanzania wataweza kufanya vizuri zaidi nchini Kenya. Mbali na uwekezaji, ushirikiano wetu kwenye sekta ya biashara nao ni mkubwa na umeendelea kushamiri siku hadi siku.

Usafirishaji wa bidhaa za Tanzania kwenda Kenya umeongezeka kutoka Tshs309.6 billioni mwaka 2017 hadi Tshs526.3 billioni mwaka 2020.

Kwa upande wa Kenya nayo iliongeza kiwango cha kuuza bidhaa zake nchini Tanzania kutoka Tshs420 billioni mwaka 2007 hadi Tshs571 billion mwaka 2020.

Hii inatusuta sisi viongozi na wanasiasa. Inatuonyesha kuwa wananchi wa nchi zetu mbili daima wako hatua mbele yetu. Wanafanya biashara zao kwa ubunifu mkubwa lakini sisi tunang’ang’ana na sheria na vikwazo na mambo kama hayo na tunawavuta

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

nyuma kidogo. Ni wakati sasa wa sisi viongozi kubadilika tuwe daraja la kuunganisha watu wetu na sio tuwe vikwazo kwao.

Mimi na ndugu yangu Rais Uhuru Kenyatta tumekubaliana kuweka utaratibu madhubuti wa kuzuia na kukabiliana na zile pilka pilka pale zinazotokea katika mipaka yetu wakati wa kuvusha biashara kwenda na kurudi katika nchi zetu mbili.

Waheshimiwa Spika, Maseneta na Wabunge mashirikiano ya uwekezaji na biashara ni sehemu tu ya mashirikiano mazuri kati ya nchi zetu. Utalii ni eneo nyingine ambayo tunapaswa kushirikiana sana. Kama nilivyogusia ekologia zetu zinaingiliana. Hivyo hivyo, ukaribu wa vivutio vyetu vya utalii na vyenyewe vinaingiliana.

Tunayo nafasi ya kunemeka pamoja ikiwa tutashirikiana katika sekta hii kuliko kushindana. Badala ya kunyang’anyana idadi ya watalii busara inatutaka tuelekeze nguvu zetu kuhamasisha mtalii aongeze idadi ya siku ambazo atazitumia nchini Kenya na Tanzania. Kwa kufanya hivyo, sote tutafaidika.

Kama alivyowahi kusema Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alisema na ninanukuu:

“Tukipoteza muda mwingi kugawana kibaba - kibaba ni kipimo cha kupimia kama mchele, ngano, sembe.” Anasema tukipoteza muda mwingi kugawana hicho tutapoteza muda mzuri sana wa kuvuna kipimo kikubwa zaidi.

Mashirikiano yetu yanashamirishwa pia na jitihada kubwa tunazochukua katika vita dhidi ya uhalifu, ujangili, ugaidi, madawa ya kulevya na uharamia Bahari ya Hindi na katika Ziwa la Victoria.

Kwa vile muhalifu wa Kenya na Tanzania wana mashirikiano mazuri basi hakuna budi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama navyo vishikamane na wawe na mashirikiano mazuri ili tuweze kulinda maeneo yetu na kushinda ushirikiano wa wahalifu.

Mashirikiano haya mazuri baina ya vyombo vyetu yamechangia sana kuwepo kwa utulivu na kutoa fursa kwa shule za kibiashara na uwekezaji kushamiri. Kenya ikiwa salama na sisi Tanzania tuko salama. Hali kadhalika, Tanzania ikiwa salama, Kenya nayo inakuwa salama.

Waheshimiwa Maspika, Maseneta na Wabunge, ujenzi wa miundo mbinu ya pamoja ni sehemu ya jitihada zetu za kuimarisha mashirikiano yetu ya kiuchumi na kimikakati. Miradi hii inajumuisha kwa uchache miradi ifuatayo: Kwanza ni ujenzi wa barabara ya lami kutoka Lamu-Mombasa kupitia Tanga-Bagamoyo hadi Dar es Salaam yenye urefu wa kilomita 454 chini ya programme ya Jumuiya ya Africa Mashariki ya kuendeleza miundo mbinu ya bara bara kwa nchi za Jumuiya ya Africa Mashariki. Katika ushorodha wa pwani - yaani coastal corridor - kwa upande wetu tuko mbioni kukamilisha ujenzi wa kipande cha Pangani-Bagamoyo na barabara za lami zenye urefu wa kilomita

ADJOURNMENT

The Speaker of the National Assembly (Hon. Muturi)

Your Excellency Hon. Samia Suluhu Hassan, the President of the United Republic of Tanzania, Speaker of the Senate, Hon. Kenneth Lusaka, Members of the National Assembly and Senators. It is now my pleasure to announce the adjournment of this House until Thursday, 6th May, 2021 at 10.00 a.m.

DEPARTURE OF HER EXCELLENCY THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA